WATAHINIWA 134,390 KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA NCHINI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

WATAHINIWA 134,390 KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA NCHINI.

JUMLA ya watahiniwa 134,390 wamesajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha sita unaotarajiwa kufanyika Mei, 5(leo) hadi 26 mwaka huu, nchini

Sophia Kingimali.
By Sophia Kingimali.
04 May 2025
WATAHINIWA 134,390 KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA NCHINI.

JUMLA ya watahiniwa 134,390 wamesajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha sita  unaotarajiwa kufanyika Mei, 5(leo) hadi 26 mwaka huu, nchini.

Katika mtihani huo watahiniwa wa shule ni 126,957 na wakujitegemea ni 7,433.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA), Dk.Said  Mohamed alisema kati ya watahiniwa wa shule waliosajiliwa , wanaume ni 64,581  sawa  na asilimia 50.87 na wasichana ni 62, 376 sawa na asilimia 49.13.

Pia watahiniwa wenye mahitaji maalumu wapo 453 ambao kati yao  300ni wenye uoni hafifu, 16 wasioona , 75 wenye ulemavu wa viungo vya mwili , wenye ulemavu  wa akili wanne na wenye uziwi 58.

Alisema kati ya watahiniwa wa kujitegemea 7,433 wamesajiliwa, wavulana  ni 4782 sawa na asilimia 64.33 na wasichana ni 2,651  sawa na asilimia 35.67 huku mtahiniwa wa kujitemea wenye mahitaji maalumu wakiwa 151 kati yao wenye uoni hafifu ni 142 na wasioona ni tisa.

Alisema kumekuwa na ongezeko la jumla la watahiniwa wa shule na kujitegemea  20,854 sawa na asilimia 18.37 mwaka huu ukilinganisha na mwaka 2024 ambapo walikuwa 113,536.

"Katika mtihani wa ualimu,  unaotarajia kuanza Mei 5, hadi 19, mwaka huu , jumla ya watahiniwa 10,895 wamesajiliwa na kati yao 3100 ni ngazi ya stashahada na watahiniwa 7775 ni ngazi ya cheti, Kwa ngazi ya stashahada wanaume ni 1751 sawa na asilimia 56.48 na wanawake  ni 1349 sawa na asilimia 43.52," alisema.

Pia, watahiniwa 3808 wa ngazi ya cheti  sawa na asilimia 48.85 ni wanaume na watahiniwa 3987 sawa na asilimia 51.15 ni wanawake, watahiniwa wenye mahitaji maalumu  waliosajiliwa  kufanya mtihani wa ualimu ni 23 kati yao wawili ni wenye uoni hafifu kwa ngazi ya stashahada na 16 wenye uoni hafifu, watatu wasioona, mwenye uziwi mmoja  na ulemavu wa viungo  ngazi ya cheti ni mmoja.

Alisema mwaka 2024, idadi ya watahiniwa wa ualimu  waliosajiliwa walikuwa 11, 435 hivyo kuna upungufu wa jumla ya watahiniwa 540 sawa na asilimia 4.72 kwa mwaka huu.


Alisema maandalizi yote ya mtihani huo yamekamilika ikiwa kusambaza mitihani  husika, vitabu vya kununua na nyaraka zote muhimu zinazohusu mtihani huo  katika Mikoa na Halmashauri.

Dk.Mohamed alisema mtihani huo ni muhimu kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla, kwani hupima maarifa, stadi na umahiri wa wanafunzi katika maeneo yote waliyojifunza kwa kipindi cha miaka miwili.

Pia baraza hilo limezitaka kamati za Mitihani za Mikoa na Halmashauri, Manispaa na majiji kuhakikisha taratibu zote za uendeshaji zinazingatiwa.

" Kamati zihakikishe  mazingira ya mitihani  yanakuwa salama, tulivu na kuzuia mianya yote inavyoweza kusababisha kutokea  kwa udanganyifu, kuimarisha usalama wa vituo teule na kuvisimamia kwa kuzingatia mwongozo uliotolewa na baraza hilo,"alisema.

Pia aliwataka wasimamizi wa Mitihani kufanya kazi kwa kusimamia Mitihani kwa kwa welidi na uaminifu wa hali ya juu kwa kuzingatia  kanuni za mtihani, taratibu na miongozo  ya Baraza la Mitihani  waliyopewa ili kila mtahiniwa apate haki yake.

Katibu huyo  alisema anaamini kuwa walimu na wakufunzi wamewaandaa vizuri katika miaka miwili  ya elimu ya sekondari ya juu na kozi ya mafunzo  ya ualimu, hivyo anatarajia kila  mtahiniwa atafanya  mtihani kwa kuzingatia  kanuni za mtihani.

" Baraza halitarajii kuona mtahiniwa yeyote kujihusisha na vitendo vya udanganyifu, mtahiniwa yeyote atakayebainika kufanya udanganyifu  matokeo yake yatafutwa kwa mujibu wa kanuni za mitihani.

Pia NECTA  imewataka wakuu wa shule na wakuu wa vyuo kutekeleza majukumu yao ya usimamizi kwa kuzingatia mwongozo wa usimamizi uliotolewa ba baraza na kuepuka kuingilia usimamizi wa watahiniwa ndani ya vyumba vya mtihani kwani halitasita kukifutia kituo chochote cha mtihani endapo litajiridhisha  pasipo shaka kuwa uwepo wake unahatarisha usalama wa mtihani.

"Baraza halitasita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayebainika kujihusisha na kusababisha udanganyifu kufanyika kwa mujibu wa sheria za nchi, alisema.

Hata hivyo mtihani wa kidato cha sita unatarajiwa kufanyika katika jumla ya shule za sekondari 982 na vituo vya watahiniwa wa kujitegemea 245 na mtihani wa ualimu utafanyika  katika vyuo vya ualimu 68.
=======

SERIKALI NA WADAU WAENDELEZA MAPAMBANO YA KIJINSIA

SERIKALI NA WADAU WAENDELEZA MAPAMBANO YA KIJINSIA

Siku Ya Utumishi wa Umma, Watumishi Kufanya Maonesho ya Kutambua Mchango na Umuhimu wao Kwenye Jamii.

Siku Ya Utumishi wa Umma, Watumishi Kufanya Maonesho ya Kutambua Mchango na Umuhimu wao Kwenye Jamii.

Vijana Kutoka Kenya Waonywa Vikali Kuacha Kumkejeli Rais Samia Katika Mitandao ya Kijamii

Vijana Kutoka Kenya Waonywa Vikali Kuacha Kumkejeli Rais Samia Katika Mitandao ya Kijamii

Wizara Imetekeleza Mradi wa Uboreshaji wa Usalama wa Milki za Ardhi(LTIP)

Wizara Imetekeleza Mradi wa Uboreshaji wa Usalama wa Milki za Ardhi(LTIP)