

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde tarehe 10 mwezi Machi 2025 amekabidhi Kompyuta 50 na Printa 50 kwa Shule za Sekondari za serikali za Dodoma Jiji pamoja na maabara ya kisasa ya Kompyuta kwa Shule ya Sekondari Viwandani na kuahidi kuifanya Dodoma kuwa kinara kwenye matumizi ya teknolojia kwenye kufundishia.
Mavunde ameyasema hayo katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo iliyofanyika Shule ya Sekondari Viwandani.
“Tunaipongeza serikali chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa maboresho makubwa ya miundombinu kwenye sekta ya elimu Jijini Dodoma ambapo kwa mwaka huu wa fedha zimetengwa Tsh 16 bilioni.
Kompyuta hizi na Printa natumai zitachochea ufaulu na kuwajengea uwezo wanafunzi wetu.
Katika Kompyuta hizi tumeweka mitihani yote ya kitaifa kuanzia mwaka 1988-2024 kwa Kidato cha II, IV,VI na QT, vitabu vya ziada na kiada,Simulation za masomo ya Sayansi,video tutorials za masomo mbalimbali na notes za masomo yote“Alisema Mavunde
Naye Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri amepongeza kazi kubwa inayofanywa na Mbunge Mavunde kwenye sekta ya Elimu na kuitaka Halmashauri ya Jiji Dodoma kuhakikisha inatenga fedha ili kuziunganisha shule zote za Dodoma na Intaneti.
Diwani wa kata ya Viwandani Jaffar Mwanyemba amemshukuru Mbunge Mavunde kwa ukarabati na kuweka vifaa vya maabara na kuwataka wanafunzi watumie nafasi hiyo kujiongezea maarifa zaidi
DKT. BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA CLIMATE INVESTMENT FUNDS
KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani
MIKOA 16 kunufaika na Nishati ya Jotoardhi
MASAA YA Upatikanaji wa Huduma ya Maji Yameongezeka Kutoka saa 16 hadi saa 22
MAMLAKA ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imefanikiwa kutoa mafunzo kwa wadau wa kemikali
Hatua Kali Za Kisheria Kuchukuliwa Kwa Watakaoghushi Cheti Cha Kuhitimu Mafunzo ya JKT.
Vituo 94 vimepewa mikopo na NHIF kwa ajili ya kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi.
RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya Migogoro ya Ardhi Nchini.
NCAA IMEFANIKIWA Kudhibiti Ujangili wa Wanyamapori Ndani na Nje ya Hifadhi ya Ngorongoro.
MAMLAKA ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imefanikiwa kutoa mafunzo kwa wadau wa kemikali