

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde tarehe 10 mwezi Machi 2025 amekabidhi Kompyuta 50 na Printa 50 kwa Shule za Sekondari za serikali za Dodoma Jiji pamoja na maabara ya kisasa ya Kompyuta kwa Shule ya Sekondari Viwandani na kuahidi kuifanya Dodoma kuwa kinara kwenye matumizi ya teknolojia kwenye kufundishia.
Mavunde ameyasema hayo katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo iliyofanyika Shule ya Sekondari Viwandani.
“Tunaipongeza serikali chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa maboresho makubwa ya miundombinu kwenye sekta ya elimu Jijini Dodoma ambapo kwa mwaka huu wa fedha zimetengwa Tsh 16 bilioni.
Kompyuta hizi na Printa natumai zitachochea ufaulu na kuwajengea uwezo wanafunzi wetu.
Katika Kompyuta hizi tumeweka mitihani yote ya kitaifa kuanzia mwaka 1988-2024 kwa Kidato cha II, IV,VI na QT, vitabu vya ziada na kiada,Simulation za masomo ya Sayansi,video tutorials za masomo mbalimbali na notes za masomo yote“Alisema Mavunde
Naye Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri amepongeza kazi kubwa inayofanywa na Mbunge Mavunde kwenye sekta ya Elimu na kuitaka Halmashauri ya Jiji Dodoma kuhakikisha inatenga fedha ili kuziunganisha shule zote za Dodoma na Intaneti.
Diwani wa kata ya Viwandani Jaffar Mwanyemba amemshukuru Mbunge Mavunde kwa ukarabati na kuweka vifaa vya maabara na kuwataka wanafunzi watumie nafasi hiyo kujiongezea maarifa zaidi
Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum
DIB YAHIMIZA WANANCHI KUDAI FIDIA ZAO KUTOKA BENKI ZILIZOFILISIKA
USHIRIKI WA TAWA KATIKA MAONESHO YA 49 YA BIASHARA YA KIMATAIFA
DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA
BoT YAWATAKA TAMFI NA TAMIU KUBORESHA UPATIKANAJI WA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA.
Aliyeongoza kura maoni Vunjo 2020, kumkabili tena Dkt. Kimei
Maiko Salali achukua fomu ya ubunge Jimbo la Mpwapwa
Serikali kufanya mageuzi ya kimtazamo katika nafasi za uongozi kwa wanawake
Dkt.Tulia Aweka Jiwe La Msingi Ujenzi wa Shule ya Wavulana Bunge.
Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma