
Hayo yamejiri Kufuatia wakazi wa maeneo mbalimbali hapa nchi kutochukua tahadhari za mara kwa mara katika kujilinda na wanyama wakali ambao ni hatarishi kwa maisha yao.
Beatus Maganja ambae ni Afisa Habari mamlaka ya Usimamizi wanyama Pori Tanzania TAWA amewaeleza wananchi hao kuwa serikali imejipanga kikamilifu ili kuhakikisha wananchi wanakuwa salama.
"katika kukabiliana na changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu Serikali inahakikisha usalama wa mwananchi unakuwa ni kipaumbele cha kwanza na ndiyo maana mara kwa mara Maofisa wa TAWA wamekuwepo maeneo mbalimbali nchini kutoa elimu na kufanya doria katika maeneo ambayo yanatajwa kuwa na changamoto ya wanyamapori hao". Amesema hayo Maganja.
Kwa upande Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Bw. Joshua Manumbu ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA kwa elimu wanayoendelea kuitoa katika jamii namna ya kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na wanyamapori wakali na waharibifu hususani mamba na viboko na kuwadhibiti pale wanapoonekana kuhatarisha maisha ya wananchi.
"Halmashauri ya wilaya ya Ukerewe imekuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na Maofisa wa TAWA kutoka Kanda Maalumu ya Mwanza na imetoa ushirikiano mkubwa kwa Maofisa hao ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ipasavyo" .amesema hayo Manumbu
Kwa upande wao, wananchi wa Kijiji cha Selema kilochopo Kata ya Bwiro wilayani humo wameipongeza na kuishukuru TAWA kwa elimu wanayoendelea kuitoa wilayani humo ambayo wamekiri kuwa imekuwa msaada kwao na itawawezesha kuendelea na shughuli zao za kiuchumi huku wakiepuka madhara yanayoweza kusababishwa na wanyamapori hao.
Mamlaka ya usimamizi wanyamapori Tanzania TAWA imekuwa ikitoa elmu maeneo mbalimbali hapa nchini lengo ikiwa ni kuwafikia wananchi wanaoishi maeneo hatarishi dhidi ya wanyama hao.
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
SERIKALI Imeendelea Kujenga na Kuboresha Miundombinu ya Viwanja vya Ndege