BUNGE Marathon kujenga shule ya Sekondari ya Wavulana. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

BUNGE Marathon kujenga shule ya Sekondari ya Wavulana.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dkt. Tulia Ackson amezindua mbio za Bunge Marathon Aprili 13,2024 katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma lengo ni kukusanya fedha kwa ajili ya kujenga Shule ya Sekondari ya Wavulana.

Moreen Rojas
By Moreen Rojas
14 Apr 2024
BUNGE Marathon kujenga shule ya Sekondari ya Wavulana.

Mbio hizo zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Kaspar Mmuya, Waheshimiwa Wabunge na Katibu wa Bunge, Nenelwa Mwihambi pamoja na wadau wa michezo.

Akizungumza kwenye bonanza hilo Spika Tulia ameeleza kufurahishwa kwake na ushiriki wa  wazee, walemavu na watoto waliojitokeza kukimbia mbio za kilometres tano hadi kilometers 10 na kueleza kuwa huo ni uzalendo unaofaa kuigwa.

Mbali na kufurahishwa na ushiriki huo ametumia nafasi hiyo kuitaka jamii kuwa na utaratibu wa kufanya mazoezi ili kuipunguzia mzigo serikali wa magonjwa yasiyo ambukizwa.

"Serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa kupambana na magonjwa hayo, jamii inapaswa kuthamini michezo,nimefurahishwa na mzee wa Miami 92 kukimbia mbio za kilometres 10 huku watoto kuanzia umri wa miaka 5 hadi 9 kukimbia mbio za kilometres 5 hongereni Sana kwa kujitoa kwenu, "amesema

Sambamba na hilo amesema marathon hiyo inalenga kuchangia ujezi wa shule ya secondary ya wavulana ambapo kila mbunge atachangia shilingi Million 3.5 huku akibainisha kwa kila mchangiajiajina yao yataandikwa kwa wino wa dhahabu na kihifadhiwa shuleni hapo

Mbio hizo za kuanzia Km 21, Km 10 na Km 5 zimeongozwa na wadau mbalimbali wakishiriki wakiwemo Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa upande wake Meya wa Jiji la Dodoma Devis Mwamfupe amesema michezo ni furaha na huleta amani  huku akimshukuru Spika wa Bunge kwa kuwa na maono ya kuwagusa Wavulana.

DKT.TULIA AMUAPISHA BALOZI KOMBO AMTAKA KUCHAPA KAZI.

DKT.TULIA AMUAPISHA BALOZI KOMBO AMTAKA KUCHAPA KAZI.

RAIS DK.SAMIA awaongoza watanzania maadhimisho ya siku ya mashujaa.

RAIS DK.SAMIA awaongoza watanzania maadhimisho ya siku ya mashujaa.

HISTORIA IMEANDIKWA SGR YAZINDUA SAFARI ZAKE RASMI DAR ES SALAAM-DODOMA.

HISTORIA IMEANDIKWA SGR YAZINDUA SAFARI ZAKE RASMI DAR ES SALAAM-DODOMA.

RAIS DKT SAMIA ASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA

RAIS DKT SAMIA ASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA

DIWANI MAKURUMLA AWATOA HOFU WAZAZI UTEKAJI WA WATOTO.

DIWANI MAKURUMLA AWATOA HOFU WAZAZI UTEKAJI WA WATOTO.