BODABODA NA MACHINGA HATUTAKUWA CHANZO KUVUNJA AMANI YETU | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

BODABODA NA MACHINGA HATUTAKUWA CHANZO KUVUNJA AMANI YETU

Makundi ya waendesha bodaboda na wamachinga yamezunguka katika mitaa kadhaa ya jiji la Dar es Salaam ikiwemo Posta, Kisutu, Kivukoni, Kariakoo, Karume, na Buguruni, yakihamasisha wananchi kulinda amani na kujitokeza kupiga kura siku ya tarehe 29 Oktoba.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
20 Oct 2025
BODABODA NA MACHINGA HATUTAKUWA CHANZO KUVUNJA AMANI YETU

Makundi ya waendesha bodaboda na wamachinga yamezunguka katika mitaa kadhaa ya jiji la Dar es Salaam ikiwemo Posta, Kisutu, Kivukoni, Kariakoo, Karume, na Buguruni, yakihamasisha wananchi kulinda amani na kujitokeza kupiga kura siku ya tarehe 29 Oktoba.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kiongozi wa waendesha bodaboda Ilala, Abdul Kimaro, amewataka vijana wenzake kutokubali kurubuniwa kufanya vurugu na badala yake kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa kupiga kura kwa amani.

Kwa upande wao, makundi ya bodaboda na wamachinga wameonesha kukubali elimu hiyo, huku baadhi yao wakiapa kujitokeza kupiga kura na kusisitiza kuwa hawatashiriki katika vurugu za aina yoyote.

Viongozi wengine wa wamachinga na wajasiriamali wadogo (mama na baba lishe) na bodaboda nao wamejitokeza kuunga mkono kampeni hiyo ya amani, wakisisitiza kuwa uchaguzi ni fursa ya maendeleo na siyo sababu ya migogoro.

CWT YATOA WITO KWA WALIMU KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU NA KUELEIMISHA JAMII KUHUSU UMUHIMU WA KUPIGA KURA

CWT YATOA WITO KWA WALIMU KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU NA KUELEIMISHA JAMII KUHUSU UMUHIMU WA KUPIGA KURA

Hakuna Maendeleo Bila Amani, Hakuna Taifa Imara Bila Mshikamano - Dkt. Judith

Hakuna Maendeleo Bila Amani, Hakuna Taifa Imara Bila Mshikamano - Dkt. Judith

AMANI NI DARAJA LA HAKI, TUITUNZE KWA GHARAMA YOYOTE- ASKOFU DKT. AKYOO

AMANI NI DARAJA LA HAKI, TUITUNZE KWA GHARAMA YOYOTE- ASKOFU DKT. AKYOO

RC MAKALLA AWAHAKIKISHIA USALAMA WAZEE WA MKOA WA ARUSHA SIKU YA UPIGAJI KURA OKTOBA 29.

RC MAKALLA AWAHAKIKISHIA USALAMA WAZEE WA MKOA WA ARUSHA SIKU YA UPIGAJI KURA OKTOBA 29.

Mfalme wa Mashairi Awasha Moto wa Uzalendo: “Kura Yako Ni Silaha”

Mfalme wa Mashairi Awasha Moto wa Uzalendo: “Kura Yako Ni Silaha”