WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO

Mahakama ya Wilaya ya Lugoba, Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani, imewahukumu watu wawili, Mayunga Senteu na Muganyi Makulu, kifungo cha miaka 20 jela kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kuiba na kuharibu miundombinu ya umeme.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
12 May 2025
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO

Mahakama ya Wilaya ya Lugoba, Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani, imewahukumu watu wawili, Mayunga Senteu na Muganyi Makulu, kifungo cha miaka 20 jela kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kuiba na kuharibu miundombinu ya umeme.

Wawili hao walikutwa na hatia ya kuiba nyaya za umeme aina ya ACSR kutoka katika laini ya umeme ya kilovoti 33 (33KV), mali ya Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme (ETDCO).

Tukio hilo lilitokea mwaka 2024 katika eneo la Chamakweza, Kata ya Vigwaza, ambapo zaidi ya span 25 za nyaya ziliibwa kutoka kwenye mradi wa ujenzi wa miundombinu ya umeme uliokuwa ukiendelea. Watuhumiwa walikamatwa wakiwa na viroba vya nyaya hizo na kufikishwa Mahakamani kwa kesi namba EC8785/2024.

Katika hukumu iliyotolewa Mei 8, 2025, Mahakama iliwatia hatiani na kutoa adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela kwa kila mmoja, ikiwa ni hatua ya kukabiliana na uharibifu wa miundombinu ya Taifa.

Waziri Mkuu Azindua Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini GovESB.

Waziri Mkuu Azindua Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini GovESB.

LUKUVI AWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA DAWA ZA KULEVYA

LUKUVI AWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA DAWA ZA KULEVYA

UDSM YASAINI MAKUBALIANO NA KAMPUNI ZA CHINA KUTOA MAFUNZO KWA VITENDO KWA WANAFUNZI WA CHUO HICHO.

UDSM YASAINI MAKUBALIANO NA KAMPUNI ZA CHINA KUTOA MAFUNZO KWA VITENDO KWA WANAFUNZI WA CHUO HICHO.

KIHENZILE:WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI FURSA MUHIMU KWA WANANCHI

KIHENZILE:WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI FURSA MUHIMU KWA WANANCHI

MOI YASEMA WAGONJWA WENGI WANAOWAHUDUMIA WANA MATATIZO SUGU.

MOI YASEMA WAGONJWA WENGI WANAOWAHUDUMIA WANA MATATIZO SUGU.