

Mahakama ya Wilaya ya Lugoba, Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani, imewahukumu watu wawili, Mayunga Senteu na Muganyi Makulu, kifungo cha miaka 20 jela kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kuiba na kuharibu miundombinu ya umeme.
Mahakama ya Wilaya ya Lugoba, Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani, imewahukumu watu wawili, Mayunga Senteu na Muganyi Makulu, kifungo cha miaka 20 jela kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kuiba na kuharibu miundombinu ya umeme.
Wawili hao walikutwa na hatia ya kuiba nyaya za umeme aina ya ACSR kutoka katika laini ya umeme ya kilovoti 33 (33KV), mali ya Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme (ETDCO).
Tukio hilo lilitokea mwaka 2024 katika eneo la Chamakweza, Kata ya Vigwaza, ambapo zaidi ya span 25 za nyaya ziliibwa kutoka kwenye mradi wa ujenzi wa miundombinu ya umeme uliokuwa ukiendelea. Watuhumiwa walikamatwa wakiwa na viroba vya nyaya hizo na kufikishwa Mahakamani kwa kesi namba EC8785/2024.
Katika hukumu iliyotolewa Mei 8, 2025, Mahakama iliwatia hatiani na kutoa adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela kwa kila mmoja, ikiwa ni hatua ya kukabiliana na uharibifu wa miundombinu ya Taifa.
Waziri Mkuu Azindua Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini GovESB.
LUKUVI AWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA DAWA ZA KULEVYA
UDSM YASAINI MAKUBALIANO NA KAMPUNI ZA CHINA KUTOA MAFUNZO KWA VITENDO KWA WANAFUNZI WA CHUO HICHO.
WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MAGEREZA NA VYUO VYA MAFUNZO WANOLEWA
MAONESHO YA UTALII NA UWEKEZAJI ZANZIBAR; FURSA KWA WANANCHI KUJUA VIVUTIO VYA UTALII VILIVYOPO NGORONGORO
GRAND BUNGE BONANZA KUFANYIKA JUNI 21 2025 HUKU MGENI RASMI AKITARAJIWA KUWA RAIS SAMIA.
CDE SALUM ATANGAZA NIA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KAHAMA MJINI.
KIHENZILE:WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI FURSA MUHIMU KWA WANANCHI
NISHATI YA GESI ASILIA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA NCHI.
MOI YASEMA WAGONJWA WENGI WANAOWAHUDUMIA WANA MATATIZO SUGU.