WANANCHI LUHITA WALIA NA MAGUGU ZIWA BURIGI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

WANANCHI LUHITA WALIA NA MAGUGU ZIWA BURIGI.

Wananchi Kijiji cha Luhita Wilaya ya Karagwe Mkoa Kagera wanaotumia Ziwa la Burigi wameliomba Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kuangalia namna ya kutoa magugu katika Ziwa hilo kutokana na changamoto wanazozipata wakati wa kusafiri na kuvua samaki na vyombo vya usafiri majini.

NICHOLAUS KINYARIRI (OUT).
By NICHOLAUS KINYARIRI (OUT).
30 Apr 2025
WANANCHI LUHITA WALIA NA MAGUGU ZIWA BURIGI.

Wananchi Kijiji cha Luhita  Wilaya ya Karagwe Mkoa Kagera wanaotumia Ziwa la Burigi wameliomba Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kuangalia namna ya kutoa magugu katika Ziwa hilo kutokana na changamoto  wanazozipata wakati wa kusafiri na kuvua samaki na vyombo vya usafiri majini.

Wananchi hao wameyasema hayo wakati ziara Bodi ya TASAC wakati walipotembelea Mwalo wa Luhita katika Ziwa Burigi kuangalia usalama wa usafiri wa majini katika Ziwa hilo.

Mwenyekiti wa Usimamizi wa  Mazingira ya Fukwe (BMU) Nelson Atanas amesema kuwa katika kufany safari katika ziwa hilo upande wa Luhita imekuwa changamoto kutokana njia wanaoitumia wamechonga ambapo  vyombo vya usafiri majini viwili haviwezi kupishana.

Amesema  ujio wa Bodi kwao ni fursa ya kuweza kupata msaada namna ya kutoa au kupunguza magugu katika mwalo huo na kurahisisha usafiri wa kwenda upande wa pili ambapo wananchi wote wanategemeana kwa biashara.

Kwa upande mwananchi wa kijiji wa Mwalo wa Luhita Leopord Baltazal amesema kuwa utafika wakati kutokana na magugu hayo kuongezeka watashindwa kufanya shughuli za uvuvi pamoja na kusafiri kwenda upande wa pili na kufanya maisha yao kuwa magumu.

Akitolea ufafanuzi wa changamoto hizo  Mwenyekiti wa Bodi ya TASAC  Nah.Mussa Mandia amesema kuwa TASAC  wanachukua changamoto  katika kufanyia kazi ili kuhakikisha shughuli zao ziendelee kutokana  na kuwa na mchango kwa mapato na maisha yao kwa ujumla.

Amesema katika kushughulika na magugu ni pamoja kuwa na gati na miundombinu mingine ya huduma katika mwalo wa Luhita.

Hata hivyo Mwenyekiti wa Bodi katika Mwalo huo amemwagiza Mtendaji wa kijiji kuandika kwa maandishi mahitaji yanayohitajika na kupeleka kwa Afisa Mfawidhi wa TASAC Mkoa Kagera.

Nahodha  Mandia amesema kuwa licha kuwa na changamoto  hizo usalama unahitajika kutokana na sheria ya kuhakikisha wanakuwa na vifaa vya uokozi wakati wote.

Amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita ya Dkt.Samia Suluhu Hassan iko karibu na wananchi katika kutatua changamoto na mengi yamefanyika kwenye Bandari ,Mialo ya Uvuvi na usafirishaji wa abiria.

Ilani Ya CCM Imeandaliwa Kwa Weledi Mkubwa Kwa Kushirikiana Na Wananchi;RAIS Dkt.Samia

Ilani Ya CCM Imeandaliwa Kwa Weledi Mkubwa Kwa Kushirikiana Na Wananchi;RAIS Dkt.Samia

KAPINGA ATAJA VIGEZO VYA ZIADA UPELEKAJI UMEME VITONGOJINI.

KAPINGA ATAJA VIGEZO VYA ZIADA UPELEKAJI UMEME VITONGOJINI.

MINARA 304 YA 2G IMEBORESHWA HADI KUFIKIA 3G/4G-UCSAF.

MINARA 304 YA 2G IMEBORESHWA HADI KUFIKIA 3G/4G-UCSAF.

SERIKALI IMETOA RUZUKU YA ASILIMIA 20 HADI 50 KWENYE MITUNGI YA GESI  LAKI 4.4 – KAPINGA.

SERIKALI IMETOA RUZUKU YA ASILIMIA 20 HADI 50 KWENYE MITUNGI YA GESI LAKI 4.4 – KAPINGA.

SERIKALI YAWATAKA WADAU KUWEKA MAZINGIRA YANAYORUHUSU UBUNIFU.

SERIKALI YAWATAKA WADAU KUWEKA MAZINGIRA YANAYORUHUSU UBUNIFU.