

Kiongozi wa ACT wazalendo Dorothy Semu ameitaka serikali kuondoa mara moja tozo zote kandamizi zinazozuia biashara ndogo ndogo kuchipua huku akitoa rai kuwa fedha za uchaguzi zisitumike kupora haki na demokrasia kwa wananchi wa nchini.
Kiongozi wa ACT wazalendo Dorothy Semu ameitaka serikali kuondoa mara moja tozo zote kandamizi zinazozuia biashara ndogo ndogo kuchipua huku akitoa rai kuwa fedha za uchaguzi zisitumike kupora haki na demokrasia kwa wananchi wa nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari Leo June 21 2025 katika mkutano wa uchambuzi wa bajeti kuu ya serikali jijini Dar es salaam Dorothy amesema serikali inarundika tozo,ushuru,kodi na ada mbalimbali kwa wananchi wenye kipato cha chini huku akiongeza kuwa bajeti haijawapa hauweni umma wa watanzania
Kwa upande wake waziri kivuli wa ACT-wazalendo na Naibu Mwenyekiti ACT wazalendo Isihaka Mchinjita ameeleza kuwa bajeti ya serikali ya 2025-2026 haijatoa nafuu kwa umma wa watanzania bali imeacha maumivu makubwa haswa kwa watu wa hali ya chini hapa nchini kwa sababu haijibu changamoto sugu zinazowakabili wananchi hao.
"licha ya changamoto ya ukosefu wa walimu katika shule za msingi na secondary bajeti haionyeshi mwanga wa kutoa ajira mpya kwa waliimu pia haijatoa kipaumbele kwenye kupunguza changamoto za gharama za matibabu,kupanda kwa gharama na mafuta,dizel na petroli ",Amesema Mchinjita.
Sambamba na hayo ameongeza kuwa deni la taifa limekuwa kubwa na athari ya deni hilo linaangukia kwenye mabega ya wananchi wanyonge na kuongeza kuwa mikopo si njia sahihi ya kuboresha maendeleo ya taifa hili bali serikali ifanye uwekezaj katika miradi mbalimbali itakayonufaisha taifa ukiwemo utekelezaji wa mradi wa gesi na kuongeza ufanisi katika bandari ili kuzikabili changamoto za kiuchumi zinazoikabili nchi
Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum
DIB YAHIMIZA WANANCHI KUDAI FIDIA ZAO KUTOKA BENKI ZILIZOFILISIKA
USHIRIKI WA TAWA KATIKA MAONESHO YA 49 YA BIASHARA YA KIMATAIFA
DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA
BoT YAWATAKA TAMFI NA TAMIU KUBORESHA UPATIKANAJI WA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA.
Aliyeongoza kura maoni Vunjo 2020, kumkabili tena Dkt. Kimei
Maiko Salali achukua fomu ya ubunge Jimbo la Mpwapwa
Serikali kufanya mageuzi ya kimtazamo katika nafasi za uongozi kwa wanawake
Dkt.Tulia Aweka Jiwe La Msingi Ujenzi wa Shule ya Wavulana Bunge.
Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma