ACT YAITAKA SERIKALI KUONDOA TOZO ZINAZOZUIA BIASHARA KUKUA . | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

ACT YAITAKA SERIKALI KUONDOA TOZO ZINAZOZUIA BIASHARA KUKUA .

Kiongozi wa ACT wazalendo Dorothy Semu ameitaka serikali kuondoa mara moja tozo zote kandamizi zinazozuia biashara ndogo ndogo kuchipua huku akitoa rai kuwa fedha za uchaguzi zisitumike kupora haki na demokrasia kwa wananchi wa nchini.

Ngonise Kahise
By Ngonise Kahise
21 Jun 2025
ACT YAITAKA SERIKALI KUONDOA TOZO ZINAZOZUIA BIASHARA KUKUA .

Kiongozi wa ACT wazalendo Dorothy Semu ameitaka serikali kuondoa mara moja tozo zote kandamizi zinazozuia biashara  ndogo ndogo kuchipua huku akitoa rai kuwa fedha za uchaguzi zisitumike kupora haki na demokrasia kwa wananchi wa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Leo June 21 2025 katika mkutano wa uchambuzi wa bajeti kuu ya serikali  jijini Dar es salaam Dorothy amesema serikali inarundika tozo,ushuru,kodi na ada mbalimbali kwa wananchi wenye kipato cha chini huku akiongeza kuwa bajeti haijawapa hauweni umma wa watanzania

Kwa upande wake waziri kivuli wa ACT-wazalendo na Naibu Mwenyekiti ACT wazalendo Isihaka Mchinjita ameeleza kuwa bajeti ya serikali ya 2025-2026 haijatoa nafuu kwa umma wa watanzania bali imeacha maumivu makubwa  haswa kwa watu wa hali ya chini hapa nchini kwa sababu haijibu changamoto sugu zinazowakabili wananchi hao.

"licha ya changamoto  ya ukosefu wa walimu katika shule za msingi na secondary bajeti haionyeshi mwanga wa kutoa ajira mpya kwa waliimu pia haijatoa kipaumbele  kwenye kupunguza changamoto za gharama za matibabu,kupanda kwa gharama na mafuta,dizel na petroli ",Amesema Mchinjita.

Sambamba na hayo ameongeza kuwa deni la taifa limekuwa kubwa na athari ya deni hilo linaangukia kwenye mabega ya wananchi wanyonge na kuongeza kuwa mikopo si njia sahihi ya kuboresha maendeleo ya taifa hili bali serikali ifanye uwekezaj katika miradi mbalimbali itakayonufaisha taifa ukiwemo utekelezaji wa mradi wa gesi na kuongeza ufanisi katika bandari ili kuzikabili changamoto za kiuchumi zinazoikabili nchi

Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum

Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum

DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA

DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA

Katimba aomba ridhaa Ubunge viti maalumu Kigoma

Katimba aomba ridhaa Ubunge viti maalumu Kigoma

SAGAFF AJITOSA KUMRITHI MAVUNDE DODOMA MJINI

SAGAFF AJITOSA KUMRITHI MAVUNDE DODOMA MJINI

Ubalozi wa Marekani waahidi kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari nchini.

Ubalozi wa Marekani waahidi kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari nchini.