

Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile (Mb), amesema kuwa uwazi na uwajibikaji ni nguzo muhimu katika kuhakikisha kuwa rasilimali za umma zinatumika kwa tija na kwa faida ya wananchi wote, huku akiwataka watumishi wa umma kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kulinda maslahi ya taifa.
Kauli hiyo imepokelewa kwa uzito na viongozi wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU waliokuwa wakishiriki maonesho hayo, wakiahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu na wizara zote katika kusimamia matumizi ya fedha na kuhakikisha miradi yote inaendeshwa kwa uwazi na kufuata taratibu.
Akizungumza leo Juni 19, 2025, katika banda la TAKUKURU kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, Mhe. Kihenzile ameeleza kuwa mwaka huu una umuhimu mkubwa kisiasa na kijamii, hivyo ni jukumu la taasisi kama TAKUKURU kuhakikisha nidhamu ya fedha inazingatiwa kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Aidha amesema kuwa Serikali haitavumilia miradi yoyote inayoisimamia iwapo itabainika kuwa na viashiria vya rushwa, akisisitiza kuwa rushwa ni kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya Taifa.
“Miradi yote tunayoisimamia kama ina harufu ya rushwa haitakamilika. Na mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi, tunawatakia heri TAKUKURU mtusimamie vizuri ili tupate viongozi bora na waadilifu,” alisema Mhe. Kihenzile mbele ya viongozi wa taasisi hiyo na wadau wengine wa sekta ya usafirishaji.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Uelimishaji Umma TAKUKURU Mkoa wa Dodoma Faustine Malecha amesema wamethibitisha kuwa wataendelea kutumia jukwaa la Wiki ya Utumishi wa Umma kutoa elimu kuhusu rushwa katika maeneo mbalimbali, na kuhamasisha wananchi kushiriki uchaguzi kwa uadilifu na bila kushawishiwa kwa rushwa.
“TAKUKURU tumekuja hapa kutoa elimu kuhusu madhara ya kutoa na kupokea rushwa tunawaelimisha wananchi ili kuhakikisha kwamba hawachagui viongozi wanaonunua nafasi kwa kutoa rushwa kwa sababu viongozi wa aina hiyo hawawezi kuwaletea maendeleo,” amesema
Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum
DIB YAHIMIZA WANANCHI KUDAI FIDIA ZAO KUTOKA BENKI ZILIZOFILISIKA
USHIRIKI WA TAWA KATIKA MAONESHO YA 49 YA BIASHARA YA KIMATAIFA
DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA
BoT YAWATAKA TAMFI NA TAMIU KUBORESHA UPATIKANAJI WA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA.
Aliyeongoza kura maoni Vunjo 2020, kumkabili tena Dkt. Kimei
Maiko Salali achukua fomu ya ubunge Jimbo la Mpwapwa
Serikali kufanya mageuzi ya kimtazamo katika nafasi za uongozi kwa wanawake
Dkt.Tulia Aweka Jiwe La Msingi Ujenzi wa Shule ya Wavulana Bunge.
Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma