RAIS SAMIA APELEKA KICHEKO KWA WANANCHI WA SONGWE | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

RAIS SAMIA APELEKA KICHEKO KWA WANANCHI WA SONGWE

Mwendo mrefu wa kufuata huduma za kijamii ikiwemo huduma ya afya, sasa utakuwa ni historia kwa Wakazi wa Wilaya ya Songwe mkoani Songwe.

The Dododma Post
By The Dododma Post
02 Dec 2024
RAIS SAMIA APELEKA KICHEKO KWA WANANCHI WA SONGWE

Tabasamu na vicheko vimetawala kwenye nyuso zao baada ya Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwaongezea nguvu katika kujenga Hospitali kubwa ya Wilaya ya Songwe.

Wakazi wa wilaya hiyo walikuwa wanatumia muda mrefu kufikia huduma bora za afya hasa zile zinazohitaji matibabu na vipimo vya kibingwa, mwendo wa zaidi ya Kilometa tano ili kufikia huduma bora ulikuwa ni jambo la kawaida kwao.

Kwa bahati njema hilo sasa halitakuwepo kwani serikali ya Rais Samia imejenga Hospital kubwa ambayo itehudumia Wananchi wote wa Songwe na Wilaya za jirani.

Aidha Rais Samia  amehakikisha Wananchi  hawapati changamoto kubwa na kusafiri kwa umbali mrefu katika kupata huduma za Afya, ambapo pamoja na kujenga  majengo bora, lakini pia ameongeza upatikanaji wa huduma za matibabu na vifaa tiba vya kisasa

Hii inamaanisha kazi inayofanywa na Rais Samia inaongea yenyewe kwa vitendo.

#KAZIINAONGEA

REA YAJIZATITI KUFIKISHA LENGO LA TAIFA KWENYE NISHATI SAFI YA KUPIKIA

REA YAJIZATITI KUFIKISHA LENGO LA TAIFA KWENYE NISHATI SAFI YA KUPIKIA

MKURUGENZI TASAC AWATAKA WANANCHI KUSOMA MASOMO YANAYOHUSU SEKTA YA BAHARI.

MKURUGENZI TASAC AWATAKA WANANCHI KUSOMA MASOMO YANAYOHUSU SEKTA YA BAHARI.

SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA MWEZI AGOSTI.

SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA MWEZI AGOSTI.

WAZIRI KIKWETE AIPONGEZA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA.

WAZIRI KIKWETE AIPONGEZA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA.

NISHATI SAFI YA KUPIKIA NI AJENDA YA DUNIA, WIZARA INAITEKELEZA KWA VITENDO - DKT. KAZUNGU.

NISHATI SAFI YA KUPIKIA NI AJENDA YA DUNIA, WIZARA INAITEKELEZA KWA VITENDO - DKT. KAZUNGU.