

Mwendo mrefu wa kufuata huduma za kijamii ikiwemo huduma ya afya, sasa utakuwa ni historia kwa Wakazi wa Wilaya ya Songwe mkoani Songwe.
Tabasamu na vicheko vimetawala kwenye nyuso zao baada ya Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwaongezea nguvu katika kujenga Hospitali kubwa ya Wilaya ya Songwe.
Wakazi wa wilaya hiyo walikuwa wanatumia muda mrefu kufikia huduma bora za afya hasa zile zinazohitaji matibabu na vipimo vya kibingwa, mwendo wa zaidi ya Kilometa tano ili kufikia huduma bora ulikuwa ni jambo la kawaida kwao.
Kwa bahati njema hilo sasa halitakuwepo kwani serikali ya Rais Samia imejenga Hospital kubwa ambayo itehudumia Wananchi wote wa Songwe na Wilaya za jirani.
Aidha Rais Samia amehakikisha Wananchi hawapati changamoto kubwa na kusafiri kwa umbali mrefu katika kupata huduma za Afya, ambapo pamoja na kujenga majengo bora, lakini pia ameongeza upatikanaji wa huduma za matibabu na vifaa tiba vya kisasa
Hii inamaanisha kazi inayofanywa na Rais Samia inaongea yenyewe kwa vitendo.
#KAZIINAONGEA
WATAALAMU WA UNUNUZI NA UGAVI WAASWA KUZINGATIA MADILI
SERIKALI IMEDHAMIRIA KUHAKIKISHA KILA ENEO LINATAMBULIKA KWA ANWANI YA MAKAZI
WAGOMBEA NAFASI YA NGAZI YA URAIS CCM KUTAMBULISHWA KWENYE MIAKA 48 YA CHAMA HICHO.
SERIKALI KUFANYA SENSA YA UZALISHAJI VIWANDA KWA MWAKA WA REJEA 2023.
AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.
MABADILIKO YA SERA YA ELIMU KUAKISI MABADILIKO YA KITAIFA NA KIMATAIFA.
RASMI UZINDUZI WA SERA YA ELIMU KUFANYIKA TAREHE 1 FEBRUARI 2025.
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.
SERIKALI IMEDHAMIRIA KUHAKIKISHA KILA ENEO LINATAMBULIKA KWA ANWANI YA MAKAZI