

Chama cha Mapinduzi CCM kimeshinda nafasi 12,150 (99.01%) kwenye nafasi ya Wenyeviti wa Vijiji katika Vijiji vyote 12271 vilivyofanya Uchaguzi huku CHADEMA ikishinda nafasi 97 (0.79%).
Akitangaza matokeo ya jumla ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa jana usiku , Waziri wa TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa amesema ACT Wazalendo imeshinda nafasi 11 (0.09%) , CUF imeshinda nafasi 10, NCCR , UMD na ADC wameshinda nafasi moja kila Chama.
“Vijiji tisa havijafanya Uchaguzi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vifo vya Wagombea baada ya uteuzi” — Mchengerwa.
Chama cha Mapinduzi 'CCM' Pia kimeshinda nafasi 62728 sawa na asilimia 98.26 kwenye nafasi ya Wenyeviti wa Vitongoji Nchini ikifuatiwa na CHADEMA ambayo imeshinda nafasi 853 (1.34%) katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
ACT Wazalendo imeshinda nafasi 150 (0.23%) , CUF imeshinda nafasi 78, NCCR nafasi 10, UDP nafasi 6, UMD nafasi mbili na ADC wameshinda nafasi moja.
Aidha amesema Vitongoji nane wagombea wake walifariki dunia uchaguzi utarudiwa ambapo 37 havikufanya uchaguzi tarehe 27 Novemba, 2024. Kati ya hivyo, vitongoji havikufanya uchaguzi kwa kuwa wagombea wake walifariki baada ya zoezi la uteuzi.
" Wagombea hao walitoka katika Halmashauri za wilaya za Kilwa (2), Nanyumbu (1), Itilima (1), Ikungi (1), Manyoni (1), Uyui (1) na Mbarali (1),”amesema Mchengerwa.
Ambapo amesema vitongoji 29 havikufanya uchaguzi kutokana na sababu mbalimbali. Vitongoji 12 vitarudia uchaguzi kwa kuwa matokeo ya wagombea yalifungana. Vilevile, vitongoji 9 vitarudia chaguzi kutokana na wagombea pekee kutopata kura za kutosheleza.
Aidha, amesema katika mtaa mmoja wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga hakupatikana mshindi kwa sababu kura za wagombea wawili zilifungana.
WATAALAMU WA UNUNUZI NA UGAVI WAASWA KUZINGATIA MADILI
SERIKALI IMEDHAMIRIA KUHAKIKISHA KILA ENEO LINATAMBULIKA KWA ANWANI YA MAKAZI
WAGOMBEA NAFASI YA NGAZI YA URAIS CCM KUTAMBULISHWA KWENYE MIAKA 48 YA CHAMA HICHO.
SERIKALI KUFANYA SENSA YA UZALISHAJI VIWANDA KWA MWAKA WA REJEA 2023.
AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.
MABADILIKO YA SERA YA ELIMU KUAKISI MABADILIKO YA KITAIFA NA KIMATAIFA.
RASMI UZINDUZI WA SERA YA ELIMU KUFANYIKA TAREHE 1 FEBRUARI 2025.
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.
SERIKALI IMEDHAMIRIA KUHAKIKISHA KILA ENEO LINATAMBULIKA KWA ANWANI YA MAKAZI