Mbunge wa jimbo la Ngara Ndaisaba Ruhoro amezidi kumwaga Fedha za udhamini kwenye mashindano ya Ligi Daraja la Nne kwa miaka mitatu mfululizo katika Wilaya ya Ngara.
Hayo yamebainishwa leo Septemba 17,2024 na Kamati Tendaji ya Chama Cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Ngara (NDFA) kwa kumpa pongezi na kumshukuru Mbunge wa Jimbo la Ngara NDAISABA GEORGE RUHORO kwa kuendelea kuwa Mdhamini Mkuu kwa miaka Mitatu mfululizo na kutoa fedha za Uendeshaji na zawadi mbalimbali za washindi wanaofanya vizuri katika Ligi Daraja la Nne Wilaya ya Ngara.
Mwaka huu 2024 kwa Bingwa,Ruhoro ametoa Ng'ombe mmoja, Tsh 500,000 na Kombe, Kwa mshindi wa pili ametoa Ng'ombe mmoja na Tsh 300,000/= wakati Mshindi wa Tatu ametoa Ng'ombe mmoja na Tsh 200,000/= sambamba na mfungaji bora wa mashindano akipewa kiasi Tasilimu cha Tsh 20,000/=, Mchezaji Bora Tsh 20,000/=, Kipa bora Tsh 20,000/= na Timu yenye nidhamu Tsh 40,000/=
"NDFA tunaendelea kumshukuru kwa Ufadhili wake wa fedha za kuendesha Mashindano, Zawadi Tasilimu na Ng'ombe. Mhe. Ndaisaba George Ruhoro umeleta chachu ya kuimarisha na kuleta ushindani wa timu zaidi ya 16 zinazoshiriki Ligi yetu kila mwaka, kuibua vipaji Chipukizi
DKT. BITEKO ataka TANESCO kuongeza kasi utekelezaji miradi ya umeme wa gridi
"Hatutawavumilia wanaochochea Machafuko Nchini" Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan
(LHRC) chatoa maelekezo kwa vyombo vya ulinzi na usalama Kufuatia mauaji ya watoto watatu wa familia moja
TRA yaahidi kuwa na usawa kwa wafanyabiashara Nchini
BRIGEDIA Jenerali Ngata Apongezwa uongozi makini SUMAJKT
VIJANA NDIO WALINZI WA NCHI HII: MEJA JENERALI RAJABU MABELE
BRIGEDIA Jenerali Ngata Apongezwa uongozi makini SUMAJKT
VIONGOZI SOKO LA MACHINGA DODOMA WASIMAMISHWA KUPISHA UCHUNGUZI
TRA yaahidi kuwa na usawa kwa wafanyabiashara Nchini
(LHRC) chatoa maelekezo kwa vyombo vya ulinzi na usalama Kufuatia mauaji ya watoto watatu wa familia moja