KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeridhishwa na kasi ya ujenzi wa daraja la Pangani.

The Dododma Post
By The Dododma Post
14 Mar 2025
KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Seleman Moshi Kakoso amesema kazi iliyofanywa kwenye daraja hilo lenye urefu wa meta 525 ni kubwa hivyo Wizara ya Ujenzi na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), wahakikishe daraja hilo linakamilika kwa wakati ili kukuza fursa za uwekezaji katika ushoroba wa fukwe za mikoa ya Tanga na Pwani.

Hakikisheni kasi ya ujenzi wa daraja iendane na ujenzi wa barabara ili vikamilike na kutoa huduma mara moja", amesema Kakoso.

Kamati hiyo inayoendelea na ukaguzi wa miradi ya kimkakati katika mkoa wa Tanga  imekagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Tanga-Pangani- Bagamoyo Km 256 ambayo ujenzi wake unaendelea.

Naibu Waziri wa  Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya ameihakikishia Kamati hiyo ya Bunge kuwa barabara ya Tanga-Pangani ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 75 itakamilika Juni mwaka huu.

" Tumejipanga kuhakikisha sehemu hii ya kwanza Tanga-Pangani inakamilika ifikapo mwezi Juni wakati daraja likitarajiwa kukamilika Disemba mwaka huu", amebainisha Naibu Waziri Kasekenya.

Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Mohamed Besta amesema ujenzi huo umegawanywa katika sehemu nne ili kuharakisha ujenzi wake.

Amezitaja sehemu hizo kuwa ni Tanga-Pangani km 50, daraja la Pangani meta 525 na barabara unganishi km 25.6, barabara ya Mkange-Mkwaja-Tungamaa km 95.2 na sehemu ya Mkange-Bagamoyo Makurunge km 73.25 ambayo usanifu wake umekamilika.

Kukamilika kwa barabara hii  kutachochea ukuaji wa uchumi, kupunguza gharama na muda wa safari, kuwezesha kufikika kwa urahisi vivutio vya utalii na kuunganisha kwa njia fupi bandari za Dar es Salaam, Tanga na Mombasa.

Sio Lazima Kila Mhitimu Aajiriwe na Serikali: Waziri Simbachawene.

Sio Lazima Kila Mhitimu Aajiriwe na Serikali: Waziri Simbachawene.

Awamu ya pili uboreshaji, uwekaji wazi wa dafatri la wapiga kura kuanza mei.

Awamu ya pili uboreshaji, uwekaji wazi wa dafatri la wapiga kura kuanza mei.

Chama Cha Mawakili wa Serikali kufanya mkutano Aprili 14-15 jijini Dodoma

Chama Cha Mawakili wa Serikali kufanya mkutano Aprili 14-15 jijini Dodoma

Shule mpya ya wavulana kugharimu zaidi ya bilioni tatu

Shule mpya ya wavulana kugharimu zaidi ya bilioni tatu

MWENYEKITI CHADEMA WILAYA YA MWANGA AMTAKA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA KUTENGUA MAAMUZI YA BARAZA KUU LA CHAMA HICHO.

MWENYEKITI CHADEMA WILAYA YA MWANGA AMTAKA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA KUTENGUA MAAMUZI YA BARAZA KUU LA CHAMA HICHO.