

Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kuwa kila nyumba, jengo, kiwanja, huduma, ofisi ama eneo la biashara linatambulika kwa Anwani ya Makazi.
Hayo yameelezwa na Waziri wa mawasiliano na teknolojia ya habari Mhe.Jerry Silaa wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya wiki ya anwani za makazi yaliyofanyika ukumbi wa jakaya kikwete jijini Dodoma.
Aidha amesema kuwa Anwani ya Makazi inaundwa na Namba ya Anwani maarufu kama namba ya nyumba; Jina la Barabara au Mtaa; na Postikodi. Postikodi ama nchi zingine zinaita Zipcode ni utaalamu wa kugawa maeneo ili kurahisisha utambuzi. Kwa hapa Tanzania mgawanyo huu umefanyika katika ngazi ya kata ambapo kila Kata ina Postikodi yake yenye tarakimu tano.
Aidha amesema Anwani za Makazi inarahisisha utoaji na upokeaji wa huduma mbalimbali ili kuchochea maendeleo ya Kiuchumi na kijamii hasa katika zama hizi ambazo Mapinduzi ya 4,5 na 6 ya viwanda yanategemea matumizi ya TEHAMA,na matumizi ya TEHAMA yanalazimu kuwa na mifumo ya utambuzi ndiyo sababu ya Serikali kuanzia mfumo huu.
" Itakumbukwa kwamba utekelezaji wa Mfumo wa Anwani za Makazi ulianza mwaka 2010 na kwa mujibu wa Mpango wa utekelezaji ulitakiwa ukamilike mwaka 2015 hata hivyo, utekelezaji wake ulikuwa wa kasi ndogo ukilinganisha na matarijio, hali iliyosababisha kuanzishwa kwa Operesheni maalumu iliyojulikana kama Operesheni Anwani za Makazi ambayo ilizinduliwa na Mheshimiwa Rais, wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 08 Februari, 2022"
"Operesheni hiyo ilifanyika nchi nzima na kusimamiwa na wakuu wa mikoa Tanzania Bara na Zanzibar"Ameongeza
Aidha ameongeza kuwa Kufuatia utekelezaji wa Operesheni hiyo, Mfumo wa Anwani za Makazi umeanza kutumiwa na baadhi ya wananchi na taasisi katika kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku; na matunda ama manufaa ya Mfumo yameanza kuonekana ambapo huduma mbalimbali zinatolewa kupitia mfumo wa Anwani za Makazi kama vile barua ya utambulisho ya kidijitali; “Navigation Services”,kuonyesha mahali “locations” . Aidha, elimu inaendelea kutolewa kuhamasisha matumizi hayo.
Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na Serikali za mitaa(TAMISEMI) Dkt.Festo Dugange akizungumza Kwa niaba ya Waziri mwenye dhamana Mhe.Mohamed Ncheregwa amesema kuwa Mfumo wa Anwani za Makazi ni nyenzo ya utambuzi ambayo inatambulisha wakazi na makazi na uwepo wa mfumo huu kwa upande wa OR-TAMISEMI ni nyenzo muhimu zaidi kwani kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Serikali za Mitaa, jukumu la kutoa majina ya mitaa lipo OR-TAMISEMI, hivyo utekelezaji wa mfumo huu unarahisisha utekelezaji wa jukumu la kutoa majina ya mitaa kama ambavyo kauli mbiu ya maadhimisho haya inavyosema “TAMBUA NA TUMIA ANWANI ZA KAZI KURAHISISHA UTOAJI NA UPOKEAJI WA HUDUMA”.
Aidha amesema Ofisi ya Rais – TAMISEMI ni mdau mkuu katika utekelezaji hususan kupitia kwa Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa ambao wana wajibu wa kuwezesha uwekaji wa miundombinu; kuhuisha taarifa; na kukusanya taarifa mpya. Lakini pia TAMISEMI ni mnufaika mkubwa katika matumizi ya Mfumo; hii ni kwa kuzingatia kwamba Mfumo unawezesha utambuzi hivyo hurahisisha utoaji na upokeaji wa huduma.
"TAMISEMI ndiyo yenye wananchi na ndiyo mtoa huduma mkuu kwa wananchi, hivyo TAMISEMI inauhitaji sana Mfumo huu na kwa sasa tulifanya majaribio ya kutoa barua kwa njia ya kidijitali ambapo jambo hilo limeonyesha kuwa la mafanikio"
DKT. BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA CLIMATE INVESTMENT FUNDS
KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani
MIKOA 16 kunufaika na Nishati ya Jotoardhi
MASAA YA Upatikanaji wa Huduma ya Maji Yameongezeka Kutoka saa 16 hadi saa 22
MAMLAKA ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imefanikiwa kutoa mafunzo kwa wadau wa kemikali
Hatua Kali Za Kisheria Kuchukuliwa Kwa Watakaoghushi Cheti Cha Kuhitimu Mafunzo ya JKT.
Vituo 94 vimepewa mikopo na NHIF kwa ajili ya kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi.
RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya Migogoro ya Ardhi Nchini.
NCAA IMEFANIKIWA Kudhibiti Ujangili wa Wanyamapori Ndani na Nje ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.