

Los Angeles. Mamlaka jijini Los Angeles nchini Marekani zimethibitisha watu 16 kufariki dunia kutokana na janga la moto wa nyika ambao unaendelea kuteketekeza maeneo mbalimbali ya jiji hilo huku idadi ya vifo ikitarajiwa kuongezeka.
Kwa mujibu wa BBC, maofisa jijini humo wamesema leo Jumapili Januari 12, 2025, kuwa wanahofia huenda shughuli ya kutambua walioungua kutokana na moto huo ikachukua wiki kadhaa kwa kutumia vipimo vya vinasaba kwani vipimo vya alama za vidole na nyuso hazitambuliki kwa urahisi kutokana na kuungua vibaya.
BBC imeripoti kuwa miongoni mwa waliofariki dunia kwa kuunguzwa ma moto huo ni pamoja na Victor Shaw ambaye alifariki akipambana kuuzima moto huo ili kuinusuru nyumba yake iliyokuwa eneo la Altadena.
Taarifa ya kifo chake imethibitishwa na familia yake kuwa mwili wa mwanaume huyo (66) ulikutwa ukiwa katika barabara inayopita karibu na yalipokuwa makazi yake huku akiwa ameshikilia mashine ya kufanyia usafi kwenye bustani.
Victor aliyekuwaakiliki nyumba hiyo kwa miaka 50 iliyopita huku akiishi na dada yake Shari Shaw, ambaye alijaribu kumshawishi Jumanne Januari 7,2025, waondoke ndani ya nyumba hiyo hata hivyo aligoma kwa madai kuwa hatoweza kuiacha nyumba yake ikateketea.
Shari ameikieleza kituo cha televisheni cha CBS, kuwa kaka yake aligoma kutoka ndani ya nyumba hiyo kwa madai kuwa anataka kupambana kuikinga dhidi ya moto huo wa nyika huku yeye akiondoka na kumuacha baada ya kuona moto unazidi kusogea kwa kasi.
WATAALAMU WA UNUNUZI NA UGAVI WAASWA KUZINGATIA MADILI
SERIKALI IMEDHAMIRIA KUHAKIKISHA KILA ENEO LINATAMBULIKA KWA ANWANI YA MAKAZI
WAGOMBEA NAFASI YA NGAZI YA URAIS CCM KUTAMBULISHWA KWENYE MIAKA 48 YA CHAMA HICHO.
SERIKALI KUFANYA SENSA YA UZALISHAJI VIWANDA KWA MWAKA WA REJEA 2023.
AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.
MABADILIKO YA SERA YA ELIMU KUAKISI MABADILIKO YA KITAIFA NA KIMATAIFA.
RASMI UZINDUZI WA SERA YA ELIMU KUFANYIKA TAREHE 1 FEBRUARI 2025.
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.
SERIKALI IMEDHAMIRIA KUHAKIKISHA KILA ENEO LINATAMBULIKA KWA ANWANI YA MAKAZI