NAMBURI AGRICULTURAL COMPANY WAJA NA MBEGU BORA ZINAZOHIMILI UKAME. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Biashara

NAMBURI AGRICULTURAL COMPANY WAJA NA MBEGU BORA ZINAZOHIMILI UKAME.

Mkurugenzi wa kampuni ya Namburi Agricultural Company ambao ni wazalishaji wa mbegu bora Dkt Mary Mgonja amewataka wakulima nchini kutumia mbegu zinazozalishwa nchini ambazo zinaviwango na zinahimili ardhi aina zote.

Sophia kingimali
By Sophia kingimali
02 Aug 2024
NAMBURI AGRICULTURAL COMPANY WAJA NA MBEGU BORA ZINAZOHIMILI UKAME.

MKURUGENZI wa kampuni ya Namburi Agricultural Company ambao ni wazalishaji wa mbegu bora Dkt Mary Mgonja amewataka wakulima nchini kutumia mbegu zinazozalishwa nchini ambazo zinaviwango na zinahimili ardhi aina zote ikiwemo ukame.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo Augost 2,2024 kwenye maonesho ya Kimataifa ya wakulima Nanenane Mkoani Dodoma amesema kampuni yao imekuwa ikizalisha mbegu zenye ubora lakini pia zinahimili mpaka kwenye ukame.

"Hapo sisi tunambegu mpaka zinazohimili kwenye ukame mbapo mkulima wa maeneo hayo anaweza kuzitumia na akafanikiwa kuvuna vizuri na kufanyabiashara",Amesema Dkt Mgonja.

Aidha ameipingeza Wizara ya kilimo kwa kushirikiana na Tosci kwa kuitangaza nchi lakini pia kuzuia uuzaji wa mbegu bandio.

"Nitoe rai kwa wakulima pia kuwa makini wakati wa kununua mbegu kuhakikisha mbegu hizo zina alama ya Tosci",Amesema.

Ameongeza kampuni ya Mamburi inafanya shughuli zake za uchakataji na uzalishaji katika mkoa wa Songwe lakini wanasambaza mbegu zao kwenye maeneo mbalimbali nchini ili kuhakikisha kila mkulima anapata mbegu hizo.

Sambamba na hayo Dkt Mgonja amewata wastaafu kutumia muda huo wa kuingia kwenye kilimo ili kuendelea kufanyakazi na kujiimarisha kiafya na kiuchumi pia.

WADAU WA UNUNUZI WAASWA KUZINGATIA MAADILI KAZINI

WADAU WA UNUNUZI WAASWA KUZINGATIA MAADILI KAZINI

TRA IMEWEZA Kushirikiana na Viongozi wa Vyama vya Wafanyabiashara Kujenga Mahusiano na Kutatua Changamoto.

TRA IMEWEZA Kushirikiana na Viongozi wa Vyama vya Wafanyabiashara Kujenga Mahusiano na Kutatua Changamoto.

Leseni 2,450 zatolewa na BoT kwa taasisi za mikopo daraja la pili

Leseni 2,450 zatolewa na BoT kwa taasisi za mikopo daraja la pili

WAZIRI MKUU WA UGANDA ASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA KUDUMU

WAZIRI MKUU WA UGANDA ASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA KUDUMU