

WAZABUNI wanaoomba zabuni za umma na kupata changamoto au kutoridhika na michakato ya ununuzi wa umma wametakiwa kuwasilisha malalamiko yao katika chombo cha Mamlaka ya Rufani za Zabuni za Umma (PPAA),ili kupata haki zao.
WAZABUNI wanaoomba zabuni za umma na kupata changamoto au kutoridhika na michakato ya ununuzi wa umma wametakiwa kuwasilisha malalamiko yao katika chombo cha Mamlaka ya Rufani za Zabuni za Umma (PPAA),ili kupata haki zao.
Akizungumza katika banda la PPAA kwenye Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa PPAA, James Sando amesema chombo hicho kipo kwa ajili ya kusikiliza na na kutoa suluhu ya malalamiko ya wazabuni itokanayo na michakato ya ununuzi wa umma.
Amesema wamepokea malalamiko yote kuhusu zabuni za umma,wanachofanya ni kusikiliza na kuyatafutia ufumbuzi na mengi wameyamaliza na haki imetendeka.
Amesema katika maonesho hayo wametembelewa na watu wengi waliopewa elimu na wengine kuelimishwa utaratibu wa kuwasilisha malalamiko yao na kusema bado elimu inahitajika kwa wananchi wengi kufahamu mifumo ya kufuata endapo wana malalamiko.
Vilevile amesema kwa sasa wazabuni wote wanaoomba zabuni za ununuzi wa umma ni lazima watumie mfumo mpya wa kielektroniki wa manunuzi ya Umma ( NeST) kama sheria inavyotaka baada ya kuwasilisha maombi yake hufanyiwa kazi na kupata majibu.
Sando amesema mfumo huo ni rafiki na rahisi kwa sababu umerahisisha utoaji huduma kwa wazabuni badala ya kuwasilisha zabuni zao ana kwa ana sasa wanawasilisha kwa mtandao na hiyo inapunguza gharama na kuokoa muda.
Pia amesema kwa sasa PPAA inakamilisha kanuni mpya za rufani za mwaka 2024.
Waziri Mkuu Azindua Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini GovESB.
LUKUVI AWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA DAWA ZA KULEVYA
UDSM YASAINI MAKUBALIANO NA KAMPUNI ZA CHINA KUTOA MAFUNZO KWA VITENDO KWA WANAFUNZI WA CHUO HICHO.
WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MAGEREZA NA VYUO VYA MAFUNZO WANOLEWA
MAONESHO YA UTALII NA UWEKEZAJI ZANZIBAR; FURSA KWA WANANCHI KUJUA VIVUTIO VYA UTALII VILIVYOPO NGORONGORO
GRAND BUNGE BONANZA KUFANYIKA JUNI 21 2025 HUKU MGENI RASMI AKITARAJIWA KUWA RAIS SAMIA.
CDE SALUM ATANGAZA NIA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KAHAMA MJINI.
KIHENZILE:WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI FURSA MUHIMU KWA WANANCHI
NISHATI YA GESI ASILIA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA NCHI.
MOI YASEMA WAGONJWA WENGI WANAOWAHUDUMIA WANA MATATIZO SUGU.