EWURA YAHAMASISHA MATUMIZI YA GESI ASILIA KWENYE VYOMBO VYA MOTO. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

EWURA YAHAMASISHA MATUMIZI YA GESI ASILIA KWENYE VYOMBO VYA MOTO.

SERIKALI kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imesema itaendelea kuhamasisha matumizi ya gesi asilia katika vyombo vya moto ikiwemo magari ili kuendeleza matumizi ya nishati safi huku wito ukitolewa kwa wawekezaji kujikita katika uwekezaji wa vituo vya gesi hiyo –CNG.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
05 Jul 2024
EWURA YAHAMASISHA MATUMIZI YA GESI ASILIA KWENYE VYOMBO VYA MOTO.

SERIKALI kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imesema itaendelea  kuhamasisha matumizi ya gesi asilia katika vyombo vya moto ikiwemo magari ili kuendeleza matumizi ya nishati safi huku wito ukitolewa kwa wawekezaji kujikita katika uwekezaji wa vituo vya gesi hiyo –CNG.

Pia,amesema wataendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhamasisha matumuzi ya nishati safi ya kupikia ili kuendana na Mkakati wa Kitaifa ambao umelenga kuhakikisha Watanzania wanahamia kwenye matumizi ya nishati hiyo ya kupikia.

Hayo yamebainishwa leo Julai 5,2024 na Meneja mawasiliano na uhusiano EWURA, Titus Kaguo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ushiriki wao katika maonesho ya 48 ya biashara kimataifa yanayoendelea Jijini Dar es salaam.

"Tunawahamasisha wawekezaji wawekeze kwenye vituo vya ujazaji wa gesi asilia ambapo utaratibu umesharekebishwa na Shirika la viwango Tanzania(TBS )kwamba kituo cha mafuta kinaweza pia kuuza gesi asilia kwenye magari". Amesema Kaguo.

Sambamba na hayo Kaguo amesema –EWURA imekusudia kutumia maonesho hayo katika kutoa elimu kuhusu huduma mbalimbali zinatolewa na mamlaka hiyo.

Amesema kupitia Maonesho hayo imekuwa fursa kukutana na wadau pamoja na wananchi kwa ujumla kutoa elimu kuhusu masuala ya petroli, umeme, gesi asilia pamoja na maji na usafi wa mazingira.

Hatua Kali Za Kisheria Kuchukuliwa Kwa Watakaoghushi Cheti Cha Kuhitimu Mafunzo ya JKT.

Hatua Kali Za Kisheria Kuchukuliwa Kwa Watakaoghushi Cheti Cha Kuhitimu Mafunzo ya JKT.

Vituo 94 vimepewa mikopo na NHIF kwa ajili ya kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi.

Vituo 94 vimepewa mikopo na NHIF kwa ajili ya kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi.

UPOTEVU Wa Maji Kwa Mwaka 2021 Ulikuwa Wastani wa Asilimia 64.

UPOTEVU Wa Maji Kwa Mwaka 2021 Ulikuwa Wastani wa Asilimia 64.

KIWANGO Cha Makusanyo ya Maduhuli ya Serikali Kimepanda Kutoka Shilingi Bilioni 624.61 hadi Bilioni 753.82

KIWANGO Cha Makusanyo ya Maduhuli ya Serikali Kimepanda Kutoka Shilingi Bilioni 624.61 hadi Bilioni 753.82

JUMLA YA MIRADI 2,020 IMEFANIKIWA KUSAJILIWA NA TIC.

JUMLA YA MIRADI 2,020 IMEFANIKIWA KUSAJILIWA NA TIC.