

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa nchi ya Msumbiji, Filipe Nyusi wanatarajiwa kuzindua maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara julai 3,2024.
Rais Dk. Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa nchi ya Msumbiji, Filipe Nyusi wanatarajiwa kuzindua maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara julai 3,2024.
Akizungumza mara baada ya kutembelea maonesho hayo WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji amesema maonesho hayo yamekuwa ya Kimataifa kwa sababu waonyeshaji kutoka nje ya nchi wameongezeka tofauti na ilivyokuwa awali.
Amesema maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) ya mwaka huu ni ya mfano wa kuigwa kwa sababu yamekidhi viwango vya kimataifa.
Waziri huyo amesema maonyesho hayo pia yatatoa fursa mbalimbali kwa Watanzania kujifunza kutoka kwa wafanyabiashara wa ndani na nje.
Aidha ameongeza kuwa nchini 26 zimeshiriki maonyesho hayo ambazo zitaonyesha bidhaa zao mbalimbali .
Dk.Ashatu amesema tayari walishawaahidi Watanzania kuwa nchini hii ni ya viwanda hivyo kwenye maonyesho hayo kuna viwanda vingi vimeshiriki lengo ni kubadilishana uzoefu.
Kwa upande wake, Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalailla amewakaribisha wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam kuhudhuria kwa wingi katikà ufunguzi wa maonyesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF).
Chalamila amesema katika ufunguzi huo kutakuwa na mabasi yaendayo kasi (UDART)ambayo yatafanya safari zake katika maneno ya Mbande,Chamazi na maeneo mengine ya mbagala lengo ni kutaka kila mwananchi aweze kufika katikà maonyesho hayo
"Maonesho haya yamebeba kauli mbiu mahususi ya kuwakaribisha wawekezaji wafike kwa wingi kuwekeza nchini ambayo inasema "Tanzania ni eneo sahihi salama kwa uwekezaji"amesema Chalamira
Akizungumzia suala la usafi katikà kipindi hicho Cha maonyesho hayo amesema wamejipanga kuhakikisha Wilaya yote ya Temeke inakuwa ni safi huku ikizingatia mabadiliko ya tabia ya nchini.
"Tunahakikisha suala la ulinzi na usalama linaimarishwa zàidi hivyo majambazi na wadokozi hawatakuwa na nafasi katikà maonesho haya pia camera tulizozifunga zitatusaidia kuwaona wahalifu wote,"amesema Chalamila.
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
SERIKALI Imeendelea Kujenga na Kuboresha Miundombinu ya Viwanja vya Ndege